WASANII WA BONGO MOVIE WAANDAMANA KARIAKOO


Wasanii wa Bongo Movie leo wameandama katika maeneo ya Kariakoo kushinikiza uuzwaji wa filamu kutoka nje kwa madai ya kwamba, yanaua soko la filamu zao hapa nyumbani.


Ni siku chache tu zimepita tangu wasanii hao wa bongo Movie kuwasilisha kilio chao kwa mkuu wa mkoa Paul Makonda juu ya kuzuiwa kwa filamu hizo za nje ambazo zinasemekana ndizo zinazoua soko la Filamu za hapa ndani. Mkuu wa mkoa Paul Makonda aliamuru kutokuingizwa kwa CD za filamu ambazo haziendani na maadili ya mtanzania kutoka nje.

Naye msanii Steve Nyerere ameonesha kuwa tofauti na kile wanachoaminishwa wasanii wenzake wa bongo movie kuwa maduka yanayouza filamu za nje yakifungwa filamu zao dndipo zitaweza kununulika
“Tunaaminishwa kwamba tukifunga maduka au tukizuia filamu za nje ndio za kwetu tutauza, uongo." Alisema Seve Nyerere

Ameongeza kwa kusema, filamu za nj zilikuwapo tangu siku za nyuma hivyo kuzuia filamu za nje si kukufanya filamu za ndani kupata soko, suluhisho ni kuboresha kazi za filamu za ndani. Pia amesema tatizo hili la kukosa soko kwa filamu za bongo kunatokana na wasanii wenyewe kuwa kibiashara zaidi kunakopelekea muda mwingine kutozingatia ubora wa filamu wanazotengeneza,
“ubora wa filamu zetu watengenezaji wameshindwa kuwa wabunifu ili watu wanunue” alisema Steve Nyerere






Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment