KUMBUKUMBU YA KIFO CHA MWANAMAPINDUZI ABEID AMANI KARUME

Abeid Amani Karume alizaliwa katika kitongoji cha Pongwe kisiwani Unguja mnamo mwaka 1905 August 4, na kuwa mtoto wa kwanza kati ya watoto watano wa Bwana Amani Karume na Bibi. Amina Bint Kadir.


Abeid Amani Karume alikuwa na kiwango kidogo cha elimu, na aliwahi kufanya kazi kama baharia kabla hajaingia kwenye siasa. Lakini pia aliondoka Zanzibar na kwenda nchini Ungereza mjini London ambako alipata elimu ya masuala ya siasa na mambo ya kimataifa, pia alipata nafasi ya kukutana na baadhi ya wanasiasa na viongozi kutoka nchi mbali mbali za Afrika ikiwemo Kamuzu Banda wa Malawi ambapo karume alikomaa kisiasa na kuwa na uwezo wa kukiimarisha chama cha Afro Shiraz Party lakini pia kuboresha mahusiano na chama cha Tanganyika National Union party (TANU).

Zanzibar ilijipatia uhuru wake wa kwanza kutoka kwa waingereza Desemba 10 1963 baada ya Zanzibar National Party (ZNP) na Zanzibar People’s Party (ZPP) kushinda uchaguzi.

Karume alikuwa Rais wa kwanza, na aliiongoza nchi ya Zanzibar baada ya mapinduzi yaliyofanyika visiwani humo kumuondoa Sultan Jamshid aliyekuwa akiitawala Zanzibar hadi mwanzoni mwa mwaka 1964 Januari, miezi mitatu badae Zanzibar iliungana na Tanganyika kutengeneza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheikh Abeid Amani Karume kuwa makamu wa rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Abeid Amani Karume alifariki siku ya Ijumaa Tarehe 7 April 1972 kwa kupigwa risasi na alizikwa Tarehe 10 April siku ya Jumatatu
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment