URUSI YAKERWA NA SHAMBULIO LILILOFANYWA NA MAREKANI NCHINI SYRIA, YAIPA ULINZI SYRIA


Marekani imeishambulia Syria kwa makombora takribani 50 katika kambi ya Homs nchini humo. Shambulio hilo limekuja kutokana na shambulio la kemikali katika mji unaodhibitiwa na waasi ambapo watu kadhaa wamepoteza maisha ikiwemo watoto, pia maafisa wa Marekani wamepanga kuchukua hatua za kijeshi kutokana na shambulizi hilo la kutumia kemikali.

Makombora hayo yamerushwa kutoka katika meli za kivita za Marekani zilizo katika bahari ya Mediterania  


Kufuatia shambulio hilo Rais wa Urusi Vladmir Putin ametangaza kuipa ulinzi wa anga nchi ya Syria baada ya Marekani kukiuka makubaliano ya kimataifa ya kuishambulia nchi hiyo. Hata hivyomshirika wa Syria Urusi alitahadharisha kabla juu ya madhara yanayoweza kutokea kutokana na hatua za kijeshi zitakazochukuliwa na Marekani.


Rais wa Marekani Donald Trump jana alionesha kusikitishwa kwake kutokana na shambulio la sumu lililofanyika jana na kuamuru kutekelezwa shambulio la makombora 50 dhidi ya Syria na kuyataka mataifa yote kuomesha vitendo vya umwagaji damu nchini humo. 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment