ZAIDI YA WATU 40,000 WANAUGUA SONONA NCHINI TANZANIA

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu leo katika maadhimisho ya siku ya Afya Duniani ambayo huadhimishwa April 7 kila mwaka duniani, ametoa takwimu ambazo zinaonesha kuwa Tanzania ina zaidi ya wagonjwa 40,000 wanaougua ugonjwa wa Sonona.


Katika maadhimisho hayo kali mbiu ya maadhimisho ya siku ya Afya Duniani mwaka huu ni “SONONA TUZUNGUMZE”

Waziri huyo amesema kulingana na Takwimu za hivi karibuni za Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa sasa Duniani kuna zaidi ya watu Milioni  kwa sasa Duniani kuna zaidi ya watu Milioni 300 wanaouguamugonjwa wa Sonona ambapo idadi hiyo imeongezeka maradufu kwa 18% toka mwaka 2005 hadi 2015. 


Kulingana na takwimu hizo Tanzania ina wagonjwa wa Sonona 41,789 kwa mujibu wa H7\ali ya Afya ya magonjwa ya aili ya mwaka 2015/2016. Pia WHO imeeleza kwamba Duniani, kati ya watu watano mmoja anaugua ugonjwa huo.

SONONA NI UGONJWA GANI
Sonona ni hali inayompata mtu kimfumo usio na mpangilio kiufahamu inayoambatana na kujihisi huzuni, hali hii inaweza kuchukua wiki mbili au zaidi.

DALILI ZA UGONJWA SONONA
  • Kukosa usingizi na hamu ya kula
  • Kupenda kukaa peke na mara nyingine kutaka kujidhuru hata kujiua
  • Kuwa na kiwango kikubwa cha msongo mkubwa wa mawazo na kukosa raha.
  • Wasiwasi, shaka kupitiliza kiasi na kuwa na hasira za haraka
  • Kulala muda mrefu
  • Uchovu na kukosa nguvu
Zipo sababu kadha wa kadha ambazo zinaweza kumpelekea mtu kupata ugonjwa huu ikiwemo, kutokea kwa majanga kama vile kuungua kwa nyumba, kubakwa, mafuriko, ugomvi katika familia na mahusiano, kufiwa, kukosa huduma za kijamii na msaada n.k

Pia wataalamu wameeleza kuwepo kwa sababu za kibaiologia, na kisaikolojia ambazo wakati mwingine huweza kusababisha mtu kuupata ugonjwa huu. 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment