MAREKANI YASEMA IKO KUFANYA MAZUNGUMZO NA KOREA KASKAZINI


Marekani imesema iko tayari kwa mazungumzo yenye lengo la kuondoa zana za nyuklia na Korea Kaskazini, lakini pia serikali ya Marekani imesema itatumia nguvu za kijeshi ikiwa itahitajika kufanya hivyo.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani Rex Tillerson aliliambia baraza la usalama la umoja wa mataifa kuwa Korea Kaskazini inalenga kufanya vitisho vya kushambulia nchi za jirani yake kwa nyuklia. Hata hivyo waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa China ambayo ni mshirika mkubwa wa Korea Kaskazini amesema makubaliano ya amani ndio njia pekee.
Marekani tayari imepeleka vikosi vya jeshi katika nchi za jirani na Korea Kaskazini ikiwemo Japan na Korea Kusini huku hofu ikitanda zaidi kwa kile kinachodaiwa Korea Kaskazini kutaka kushambulia nchi hizo za jirani, na kupelekea waziri wa mambo ya nje wa Marekan Bw. Rex kuzitaka nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuiwekea vikwazo nchi ya Korea Kaskazini.
“Ni wakati wetu kuchukua hatua na kudhibiti hali hii, tishio la Korea Kaskazinila kufanya shambulio la nyuklia dhidi ya Korea Kusini au Japanlinaweza kutokea” alisema TIllerson  



Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment