Mgomo wa mabasi ambao ulikuwa
ufanyike kuanzia kesho April 4 umesitishwa na mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa
Nchi Kavu na Majini, SUMATRA baada ya madai ya chama cha wamiliki wa mabasi ya
abiria TABOA kusikilizwa na kufikia muafaka wa kurekebisha baadhi ya vipengele
vya sheria vinavyofunganisha makosa kati ya dereva na mmiliki wa chombo cha
usafiri.
Mkurugenzi mkuu wa SUMATRA,
Gilliard Ngewe amesema kusitishwa huko kwa mgomo kumetokana na kikao cha waziri
wa Mawasiliano, Uchukuzi na Ujenzi, Prof. Makame Mbarawa kuhusu kutenganishwa
kwa makosa ya dereva na mmiliki wa chombo cha usafiri.
Bw, Ngewe amesema, kanuini
hizo zitaandikwa ndani ya siku 74 katika rasimu hiyo na, wadau wa usafirishaji wametakiwa
kuendelea na shughuli za usafirishaji, na kwamba baada ya kufanya marekebisho
ya rasimu ya kanuni itarudishwa kwa wadaukuweza kujadiliwa kwa ajili ya
kuwasilisha bungeni.
Makamu Mwenyekiti wa
wamiliki wa Mabasi TABOA, Abdallah Mohamed amesema wamekubaliana na SUMATRA
kurekebishwa kwa baadhi ya kanuni za makosa kati ya wamiliki na madereva wa
mabasi.
0 comments:
Post a Comment