WATU 300 WAFARIKI KUTOKANA NA MAPOROMOKO

Huko mjini Mocoa nchini Colombia watu  300 wamepoteza maisha katika wilaya 17 zilizoko mjini Mocoa huko nchini Colombia kutokana na maporomoko  huku nyumba kadhaa  zikiwa zimeharibika.


Inaelezwa kwamba maji ambayo yalikuwa yameambatana na matope na mawe yameondoa kila kitukilichokuwa katika maeneo hayo huku makazi ya watu yakiwa yamethirika zaidi.


Rais wa Colombia Juan Manuel Santos ametembelea eneo la tukio na amesema watapanga mpango wa kusaidia wakazi wa maeneo yaliyoathirika, amoengeza kwa kusema atafanya chochote kitakachowezekana kuhakikisha wote waliopoteza maisha kwenye maafa hayo watazikwa kwa heshima na taratibu zinazotakiwa huku akitangaza hali ya tahadhari katika maeneo hayo.
Wilaya ya San Miqeuel imeathirika zaidi hadi kufikia kutoweza kutambulika. Eya wa Mocoa, Jose Antonio Castro amesema wakazi wa maeneo hayo walionywa juu ya kuchukua tahadhari ya kuhama maeneo hao japo wengi wao hawakufanya hivyo.

Jeshi la Colombia likishirikiana na kikosi cha msalaba mwekundu wanafanya jitihada za uokoaji na utoaji misaada ya haraka ikiwemo huduma ya kwanza kwa walionusurika na maporomoko hayo.

Pia Chanselor wa Ujerumani Angela Merkel ameeleza masikitiko yake na kutoa pole, Jumapili msemaji wa serikali ya Ujerumani Georg Streiter akiwa mjini Berlin alisema Chansela Merekel amesikitishwa na maafa hayo.  

.   
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment