MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA ZAHARIBU BARABARA KATIKA JIMBO LA CHALINZE

Mvua zinazoendelea kunyesha nchini zimeendelea kuleta maafa kwa wananchi, ambapo wilayani Chalinze mvua ambayo imeambatana na upepo mkali imeharibu barabara katika eneo la Buyuni na kukwamishwa shuhuli za mawasiliano na usafiri kwa wakazi wa kata ya Vigwaza na Mwavi katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Chalinze Mhe. Ridhiwani akitazama barabara ya Vigwaza-Mwavi ambayo imeharibiwa na mvua 

Kutokana na adha hiyo wakazi wa Vigwaza na Mwavi wamelazimika  kuvushwa na watu ambao wanawabeba mgongoni kwa gharama za Tsh. 2,000 hadi  3,000 ambazo ni kubwa kwa wakazi wa maeneo hayo, lakini pia magari yameshindwa kupita katika eneo hilo kutokana na uharibifu huo mkubwa.

“Barabara ni mbovu kama mnavyoiona, haipitiki, watu tunapata shida kufuata mahitaji ya nyumbani, tatizo ni mkandarasi, barabara iimejengwa bila kuwekwa makaravati” alisema Zainab Zuber mmoja wa wakazi wa maeneo hayo  aliyekuwa njiani kuelekea Mwavi.  

Hata hivyo adha hiyo imeleta neema kwa baadhi ya vijana wa maeneo hayo ambao waliitumia adha hiyo kama fursa kwa kufanya kibarua cha kuwavusha watu tangu April 7 ambapo mvua zilianza kunyesha, mmoja wa vijana hao Rashid Juma alisema wanavusha watu kwa maelewano kulingana na uwezo wa mtu

“Tunapata fedha kulingana na kichwa cha mtu au pikipiki, kila mtu mmoja 3,000 au 2,000 na pikipiki 5,000” alisema Rashid

Baadhi ya wakazi wanaotumia barabara ya Vigwaza-Buyuni wakipita katika barabara hiyo kwa shida kutokana na uharibifu uliotokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo hayo


Mbunge wa jimbo la Chalinze, Mhe. Ridhiwani Kikwete alitembelea eneo hilo na kujionea athari ambazo zimezotokea katika eneo hilo kutokana na mvua. Ridhiwani alisema hali iliyopo inawapa wakati mgumu wakazi wa maeneo hayo na kuahidi kuifikisha kero hiyo bungeni na katika halmashauri ya wilaya ya Chalinze ili lifanyiwe kazi. 

Mbunge wa Chalinze Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na waandishI wa habari juu ya uharibifu uliotokana na mvua ziazoendelea kunyesha jimboni kwake.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment