Mbunge wa Mtama
Mhe. Nape Nnauye ameeleza sababu iliyomfanya aangue kilio mbele ya wananchi
wake wa jimbo la Mtama jana alipokuwa katika mkutano wake na wananchi wa Mtama.
Mbunge huyo amesema kwamba
alishindwa kujizuia pale alipoona akina mama wamejipanga wakiwa wamelala chini
na kumtaka atembee juu yao, kitendo hiko kwa jamii za watu wa kusini kinaelezwa
ni kitendo cha heshima kubwa ambayo huoneshwa mtu, na huchukuliwa kuwa ni
dharau kubwa na wanajamii endapo mtu atatakiwa kufanya hivyo na akakataa.
“Kwa mila za kusini tendo
hili ni la heshima kimila na ukikataa ni sawa na dharau kubwa kwa
waliokufanyia, hivyo ndio maana nililizwa” ameandika Nape
0 comments:
Post a Comment