Waziri wa mambo ya ndani
Mhe. Mwigulu Nchemba na naibu waziri wake Eng. Masauni leo jijin Dar es salaam wameshiriki
katika shuhuli ya kuaga miili nane ya askai polisi ambao waliuawa siku ya
Alhamis Kibiti mkoani Pwani, ambapo paoja na hilo waziri Mwigulu amewatangazia
kiama wote waliohusika kwenye mauaji ya askari hao.
Waziri wa mambo ya ndani,
Mhe. Mwigulu Nchemba akitoa heshima za mwisho alipokuwa akiaga miili nane ya
askari polisi leo jijini Dar es salaam, kulia kwake ni naibu wake Hamad Masauni
|
Waziri Mwigulu amezungumza
hayo alipokuwa akiaga miili hiyo jijini Dar es salaam, ameongezea kwa kusema
kuwa watu hao watakamatwa wote na kufikishwa kwenye vyombo vya sharia
“Kitendo hiki cha mauaji
kilichofanyika dhidi ya askari wetu hakivumiliki hata kidogo waliohusika
tutawatafuta na kuwakamata” alisema Waziri Mwigulu
Pia aliwaomba wananchi
wanaoishi katika maeneo hayo kutoa ushirikiano kwa polisi ili kuweza kuwabaini waliohusika
na tukio hilo. Ameitaka wizara kutoa fidia kwa ndugu wa askari hao na majeruhi
bila kuwacheleweshea
“Naomba fidia kwa askari
hawa tuliowapoteza wakitumikia taifa itolewe kwa haraka bila kucheleweshwa”
alisema Waziri Mwigulu
Waziri wa mambo ya ndani,
Mhe. Mwigulu Nchemba akiwafariji wafiwa kwa kuwapa pole katika shuhuli ya kuaga
miili nane ya askari polisi leo jijini Dar es salaam
|
Mkuu wa jeshi la Polisi Nchini (IGP) Ernest Mangu ametoa onyo kwa wale wote ambao wamekuwa wakishabikia matukio kama haya katika mitandao ya kijamii, nna endapo watabainika watakamatwa mara moja, pia alisema kuwa wananchi wa eneo hilo wanafahamu waliohusika kwenye tukio hilo na kuwataka washirikiane na polisi ili watuhumiwa wote wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya dola.
Askari polisi waliopoteza
maisha katika tukio hilo ni pamoja na Mkaguzi Msaidizi Peter Kiguu, Koplo
Francis, PC Haruna, PC Jackson, PC Zakaria, PC Siwale, PC Maswi na PC Ayoub.
0 comments:
Post a Comment