Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo April 5, amewaapishwa viongozi mbali
mbali ambao amewateua, tukio hilo limefanyika Ikulu jijini Da es salaam.
Viongozi ambao wamekula
kiapo ni pamoja na Leonard Douglas Akwilapo kuwa katibu mkuu wa wizara ya
Elimu, Sayansi na Technolojia, Prof. Kitila Mkumbo ameapishwa kuwa katibu mkuu
wizara ya Maji na Umwagiliaji, Dkt. Ave Maria Emilius Semakafu ameapishwa kuwa
Naibu katibu mkuu wizara ya Elimu, Sayansi na Technolojia, Mhe. Baraka Haran
Luvanda ameapishwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe Sylvester Mwakinyuke
Ambokile ameapshwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Bw. Charles
Edward Kichele ameapishwa kuwa Kamish7na mkuu wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akimuapisha Bwana Charles Eward Kichere kuwa kamishna mkuu wa mamlaka ya mapato
Tanzania (TRA)
|
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akimuapisha Prof. Alexander Kitila Mkumbo kuwa katibu mkuu wa wizara ya Maji na
Umwagiliaji
|
0 comments:
Post a Comment