RAIS MAGUFULI AZINDUA MABWENI YA WANAFUNZI UDSM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo April 15 amezindua mabweni ya wanafunzi katika chuo kikuu cha Dar es salaam, ambapo mabweni hayo yatahudumia jumla ya wanafunzi 3,840 ambapo ni sawa na uwiano wa wanafunzi 192 kila jengo


Rais Magufuli amesema Tanzania inaweza, hii imeoneshwa baada ya mabweni hayo kukamilika ndani ya miezi nane. “Tukiamua tunaweza tukafanya watu wakaona miujiza” alisema Magufuli

Pia ameongeza kwa kusea watu walibeza kuwa Shilingi Bilioni 10 hazitoshi kujenga mabweni hayo na yasingeweza kujengwa na watanzania. Amesema mafanikio hayo yawe fundisho kwa viongozi wa serikali kutotoa fedha kwa wakandarasi wa nje na kuwaacha wa ndani ambao gharama zake ni nafuu.

Makamu mkuu wa chuo cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandara amesema mabweni hayo yana jumla ya majengo 20 yenye ghorofa nne kila moja na jumla ya vyumba 12 katika kila ghorofa.

Pia Profesa Rwekaza amesema kuwa chuo chake kimechangia ujenzi wa mabweni hayo kwa utengeneza vitanda 1,920, droo 1,920, meza 1,920, magodoro 3,840 na vitanda 3,840
  “Tutahakikisha kuwa huduma zote muhimu kama vile cafeteria ya chakula, maduka kwaajili ya mahitaji mbalimbali, zahanati, salon, kituo cha polisi na nyinginezo vinapatikana hapa hapa,” alisema Profesa Rwekeza


Aliongeza kuwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga taifa, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na. Mawaziri wote wa wizara hizo, Profesa Makame Mbarawa, Dr. Hussen Mwinyi na Profesa Joyce Ndalichako walikuwepo.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment