Wapiganaji zaidi ya 90 wa
kundi la Islamic State waliuwawa na bomu ambao lilidondoshwa na majeshi ya Marekani
siku ya Alhamis April 13 katika mapango ambamo wapiganaji hao hujificha.
Taarifa hizo zimetolewa na maafisa wa usalama wa nchini Afghanstan ambapo idadi
hiyo ni mara mbili ya ile iliyokadiriwa awali.
Kikundi cha wapiganaji cha
Islamic State kimekanusha taarifa hizo na kusema kuwa hawakumpoteza mtu yeyote
kutokana na bomu hilo lililolenga katika mapango na mahandaki ya chini
Mashariki mwa Afghanistan.
Naye Kamanda wa jeshi la
Marekani nchini Afghanistan, Jemedari John Nicholson, aliema kwamba Marekani
ilitumia bomu hilo kubwa kutokana na mbinu madhubuti ya kijeshi.
0 comments:
Post a Comment