SERIKALI KUAJIRI MADAKTARI 500 WALIOTAKIWA KWENDA KENYA

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameamuru madakrati walioomba nafasi mia tano za kwenda kuhudumu kazi ya udaktari nchini Kenya waajiriwe.


Agizo hilo limetoka mara baada ya Mahakama ya Kenya kukubali ombi lililopelekwa mahakamani na chama cha Madaktari nchini humo la kuzuia kuajiriwa madaktari kutoka nje badala yake kutimiza madai yao. Kukubaliwa kwa ombi hilo kulipelekea Rais wa Kenya Uhuru Kenyata kukubali kusaini maombi na mahitaji ya madaktari wa nchi hiyo ya kuongezewa mishahara na kuboreshewa mazingira ya kazi.

"Serikali ya Tanzania itakuwa tayari kushughulikia upya ombi la Serikali ya Kenya kupatiwa Madaktari 500, pale ambapo hakutakuwa na vikwazo vya kupeleka Madaktari wetu nchini Kenya," amesema Bi Mwalimu.


Pia waziri Ummy Mwalimu amesema madaktari hao watapangiwa vituo vya kazi na taarifa itatangazwa katika tovuti ya wizara, ikijumuisha wataalamu wengine 11 waliopokea maombi yao na kukidhi mahitaji. 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment