SERIKALI YATOA TAARIFA YA KUMUONDOA MKURUGENZI WA UNDP NCHINI BI. AWA DABO

 Bi. Awa Dabo
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeliagiza Shirika la Umoja wa Mataifa la program ya Maendeleo (United Nation Development Programs-UNDP) kwa upande wa Tanzania kumuondoa nchini Mkurugenzi wa Shirika hilo Bi. Awa Dabo
Serikali imefikia uamuzi huo kutokana na Bi. Dabo kutokuwa na maelewano mazuri na baadhi ya watumishi wenzake na menejimenti ya shirika hilo na kupelekea kuzorota kwa utendaji wa shirika hilo hapa nchini.
Baada ya kuthibitishwa kuondoka kwa mkurugenzi huyo, serikali kupitia wizara ya mambo ya nje imetoa rai kwa UNDP kuwakumbusha watumishi kuwa kipaumbele chao ni kufanya kazi na serikali ili kufikia malengo ya mpango wa maendeleo endelevu.  




Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment