MAREKANI YAPELEKA NYAMBIZI AINA YA USS MICHIGAN KOREA KUSINI


Meli ya kivita ya Marekani aina ya nyambizi yenye kuendeshwa kwa nguvu za nyuklia imewasili katika bandari ya Busan, Korea Kusini wasiwasi ukiongezeka kuhusu uwezekano wa Korea Kaskazini kufanya jaribio jingine la kombora au silaha za nyuklia.
Nyambizi hiyo, aina ya USS Michigan ni moja kati ya nyambizi mbili zinazobeba makombora yanayoendeshwa kwa nguvu za nyuklia katika jeshi la wanamaji la Marekani, pia nyambizi h7=iyo ina uwezo wa kubeba makombora ya 154 Tomahawk na meli nyambizi nyingine ndogo pamoja na wanajeshi 60,

Meli hiyo inayojulikana kwa jina USS Michigan, ambayo ina uwezo wa kushambulia kwa makombora, inatarajiwa kujiunga na kundi jingine la meli za kivita zinazoelekea eneo hilo, zikiongozwa na meli kubwa ya kubeba ndege ya Carl Vinson.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment