UHUSIANO KATI YA URUSI NA MAREKANI WADHOOFIKA

Uhusiano kati ya Marekani na Urusi umedhoofika zaidi tangu Donald Trump apate urais mwezi Jabuari mwaka 2017. Hayo yamedhihirishwa na rais wa Urusi Vladmir Putin alipokiambia kituo kimoja cha runinga kuwa imani kati ya nchi hizo mbili imepungua.


Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa nchi ya Urusi Sergei Lavrov alikutana na waziri wa mambo ya nje wa Marekani Rex Tillerson siku kadhaa huko mjini Moscow, ambapo kumekuwa na misukosuko kuhusu shambulio la kemikali nchini Syria.

Marekani ilifanya shambulio la makombora takriban 50 nchini Syria kwa kile walichokidai kuwa kuipinga majeshi ya Syria ambayo ilifanya shambulio la sumu, shambulio hilo lilipingwa vikali na Urusi, na rusi ikatangaza kuisaidia Syria katika ulinzi wa anga lake.

Naye Marekani imeitaka Urusi kuacha kuiunga mono seriakli ya Syria.


Mashambulizi ya Marekani yamezua utata kuhusu sera za Marekani nchini Syria huku baadhi ya maafisa wakitaka hatua kuchukuliwa dhidi ya Rais Assad.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment