WENGER ASEMA SPURS ILISTAHILI USHINDI

Bosi na Kocha wa Timu ya Arsenal Arsene Wenger  amesema Tottenham ilistahili ushindi katika mechi iliyochezwa leo April 30 kati ya Arsenal na Tottenham ambapo Tottenham imeigaraza timu ya Arsenal kwa Magoli mawili kwa bila

Arsene Wenger  aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na BBC mara baada ya mchezo huo kuisha “tumepoteza mchezo huu, na itatuchukua muda kujiweka sawa, lakini kiujumla Tottenham walistahili ushindi, inatubidi tukubali na tulitafakari zaidi, japo inakatisha tamaa lakini lengo letu la mwanzo katika msimu huu ni kushinda katika ligi” Alisema Wenger
Timu ya Tottenham ilijipatia ushindi wake kupitia wachezaji wake machachari kabisa Harry Kane na Dele Alli na kuweka historia ya kuwa juu nafasi nne zaidi ya timu ya Arsenal katika msimamo wa ligi kuu Uingereza, ambapo hivi sasa Spurs ikishika nafasi ya pili kwa jumla ya Pointi 77 huku Arsenal ikiwa na pointi 60.

Naye meneja wa timu ya Tottenham Spurs Mauricio Pochettino alizungumza haya,  “huu ulikuwa mchezo muhimu sana na wachezaji wameonesha mchezo mzuri, nimefurahishwa”, “tulikuwa vizuri katika kipindi cha pili, tuliweka nguvu kubwa na kutengeneza nafasi zaidi”
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment