Mwanasheria maarufu nchini Tanzania Albert Msando
ameomba radhi kufuatia video inayosambaa mitandaoni ikionesha Mwanasheria huyo
akiwa na Gigy Money ndani ya gari, ambapo Albert ameonekana akimpapasa mwanadad
huyo Gigy alipokuwa akicheza muziki kwa madoido.
Msando ameandika hayo kwenye ukurasa wake wa Instagram na kusema kwamba akikaa kimya atakuwa manafiki
kwa kuwa kitendo alichokifanya hakiwapendezi wengi kwani kimewakwaza na
kuwaangusha watu wengi japo alisema yeye ni binadamau ingawa wapo watu ambao
wanaweza kuhukumu kwa haraka zaidi.
“Nikikaa
kimya nitakua mnafiki. Nimekosea. Kilichotokea hakikupaswa kutokea. I will be a
man enough and say sorry kwa wote ambao nimewakwaza na kuwaangusha. Am so
sorry. But the beauty of all this is we all are human. Kuna watu ambao wamekuwa
wepesi kuhukumu. Siwalaumu. Ni sawa na ni haki yao. I made a stupid mistake. I
take full responsibility. Mwisho wa siku maisha lazima yaendelee. It could have
been worse. And to all those who took time to text I appreciate. Thats
friendship” ameandika Albert.
0 comments:
Post a Comment