KENYA KUANZA KUTUMIA MIFUGO NA MIMEA KAMA DHAMANA YA KUPATIA MIKOPO

Huko nchini Kenya Rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta amesaidini muswada utakaowawezesha wananchi wake kukopa kwa kutumia mifugo, mimea na vitu vya nyumbani kama dhamana ya kupata mikopo. Muswada huo umewalenga wale ambao hawana umiliki wa gari, ardhi ama nyumba kama dhamana ya kupata mkopo.

Sheria hiyo itakayojulikana kama “Movable Property Security Act 2017” itatoa fursa ya usajili wa mali ambazo zitatumika kama dhamana ya kupatia mkopo benki, kutokana na kwamba benki zimekuwa zikikataa kutumia mali zinazohamishika kama dhamana ya kupatia mikopo kutokana na kutokuwepo kwa taarifa sahihi za mali hizo zitakazwawezesha kudai mali hizo pindi mdaiwa atakaposhindwa kulipa mkopo.

Rais Kenyata amesema sharia hiyo italeta udhibiti wa uhakika kwa kutoa dhamana ya mali lakini pia itabainisha ni mali gani itafaa kutumika kama dhamana.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment