MAMIA WAJITOKEZA KUAGA MIILI YA WANAFUNZI 32 MKOANI ARUSHA

Maelfu ya wakazi wa jiji la Arusha wamehudhuria shughuli ya uagaji miili ya wanafunzi 32 wa darasa la saba, walimu wawili na dereva wa shule ya Lucky Vicen katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha waliopata ajali ya gari katika eneo la Rhotia Marera wilyana aratu walipokuwa wakisafiria kwenda shule ya jirani iitwayo Tumaini kwa ajili ya kufanya mitihani ya ujirani mwema.

Shughuli hiyo iliyoongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa niaba wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli.
Mkamu wa Rais amewaomba wananchi katika kuwaombea marehemu Mung4u awaaze mahala pema peponi a kuwafariji wafiwa katika wakati huo mgumu. Lakini Pia Makamu wa Rais amewahakikishia ndugu na wanafamilia wa marehemu kuwa serikali iko pamoja nao.

Makamu wa Rais katika hotuba yake amaeitaka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Polisi, walimu wazazi na walezi kuhakikisha sharia za usalama barabarani zinafuatwa na kuzingatiwa ili kulinda watoto pale wanapokuwa katika vyombo vya usafiri. Piaa amewataka madereva nchini kuzingatia sharia za usalama barbarani na kuacha tabia za ulevi  wa kutumia pombe na dawa za kulevya ili kuepusha kutokea kwa ajali za mara kwa mara.


Shughuli hiyo imehudhuriwa na viongozi mbali mbali wakiwemo viongozi wa kidini na kiserikali, akiwemo Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Rais wa Pili wa Serikali ya Zanzibar Mohamed Aboud na viongozi wengine wa vyama vya siasa na dini mbalimbali. 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment