NAHODHA WA SIMBA SC JONAS MKUDE APATA AJALI MKOANI MOROGORO

Kiungo wa timu ya mpira wa miguu Simba Sposts Club Jonas Mkude amenusurika kifo kufuatia ajali ya gari iliyotokea leo katika eneo la Dumila Mkoani Morogoro akitokea Dodoma kwenda Dar. Nahodha huyo wa timu ya Simba SC amepatiwa huduma ya kwanza na kuwahishwa hospitalini jijini Dar kwa matibabu zaidi.


Ajali hiyo imetokea baada ya tairi la nyuma la gari aina ya Toyota VX yenye namba za usajili T 834 BLZ waliyokuwa wakisafiri,  kupasuka na kuacha njia, majeruhi wengine wawili wamekimbizwa katika hospitali ya mkoa wa Morogoro kwa matibabu 

Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment