RAIS MAGUFULI ATOA MSAADA WA MAGARI MATATU YA KUBEBEA WAGONJWA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, John Pombe Magufuli ametoa msaada wa magari mapya aina ya Land Cruiser kwa ajili ya kubebea wagonjwa kwa wabunge watatu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa lengo la kuwasaidia wananchi wa maeneo wanayoyaongoza. 
Katibu kiongozi mkuu Mhe. Balozi John Kijazi akimkabidhi Mbunge wa Nkasi Kaskazini Ally Keissy fungu ya gari kwa ajili ya kubebea wagonjwa jimboni kwake 
Katibu mkuu kiongozi Balozi JoHn Kijazi amekabidhi magari hayo  kwa niaba ya Rais Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam kwa Mbunge wa Nkasi Kaskazini mkoa wa Katavi Mhe. Ally Keissy, Mbunge wa viti maalum mkoa wa Tabora Mhe. Munde Tambwe na Mbunge wa viti maalum mkoa a Shinyanga Mhe. Lucy Mayenga.
Akizungumza baada ya kukabidhi magari hayo Balozi Kijazi amesema Mhe. Rais Magufuli ametoa magari hayo baada ya kuguswa na kilio cha muda mrefu cha wabunge hao waliokuwa wakiomba wananchi wao wapatiwe magari  ya wagonjwa.
“Mhe. Rais ameamua kuwakabidhi nyinyi haya  magari kutokana na vilio vyenu ambavyo amekuwa akivisikia mara kwa mara, Mhe Keissy amekuwa hata akitafuta miadi ya kuja kumuona Mhe. Rais kwa suala hili, Waheshimiwa wabunge wamekuwa wakiyazungumza haya kwa muda mrefu”
Wabunge hao walimshuru Rai wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa msaada huo wa magari kwa ajili ya kubebea wagonjwa na kusema kuwa Rais ameonesha upendo na kuwajali wananchi wake kwa kutekeleza yale aliyoahidi
“Kwa wananchi na wanamkoa wa Shinyanga hususani akinamama wa mkoa wa Shinyanga mimi kama mwakilishi wao mbunge wa viti maalum mkoa wa Shinyanga nasema namshukuru sana Mhe Rais anaendelea kutekeleza yale ambayo anayoyaamini na anaendelea kuonesha upendo wake mkubwa sana kwa wananchi kwa vitendo” alisema Lucy Mayenga 



Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment