Meneja wa timu wa timu ya Chelsea Antonio Konte amesema
wachezaji wake wa timu ya Chelsea wana nafasi nzuri ya kushinda ligi ya
Uingereza katika msimu huu.
Timu ya Chelsea imepata matumaini hayo baada ya mchezo
uliochezwa jana kati yao na Middlesbrough na kushinda bao tatu kwa bila na
kuiwezesha timu hiyo kupata jumla ya point 84 wakiwa wanaendelea kuongoza ligi
hiyo ya Uingereza.
Konte aliiambia BBC katika mechi hiyo kuwa japo huu ni
msimu wa kwanza kwake na umekuwa na ushindani mkali katika ligi hiyo lakini
wchezaji wake wameonesha kwamba wanastahili kushinda ligi msimu huu
“huu ni msimu wangu wa kwanza, na umekuwa na ushindani
mkali,nimefurahishwa na wachezaji wanastahili, tumeonesha kwamba tunastahili
kushinda ligi” alisema Konte
0 comments:
Post a Comment