RAIS MAGUFULI ATUMA SALAM ZA RAMBI RAMBI KUFUATIA AJALI ILIYOTOKEA MKOANI ARUSHA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametuma salamu za rambirambi kwa mkuu wa mkoa wa Arusha Ndg. Mrisho Gambo kufuatia ajali ya basi iliyotokea leo saa tatu asubuhi katika eneo la Rhotia Marera wilayani Karatu na kusababisha vifo vya wanafunzi wa darasa la saba 32, dereva na walimu wawili wa Shule ya Lucky Vicent iliyoko mkoani Arusha.

Wanafunzi na walimu hao walikuwa wanatoka shuleni kwao na kwenda shule ya msingi Tumaini kwa ajili ya kufanya mtihani wa ujirani mwema na walipofikka eneo la Rhotia Marera basi walilopanda liliacha njia na kasha kutumbukia kwenye Korongo na kusababisha vifo hivyo. 

Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment