TUMBUA TUMBUA NDANI YA CCM BADO INAENDELEA

Chama cha Mapinduzi kimesema kuwa zoezi la kuwafukuza wasaliti kwenye chama hiko kwa sasa linakwenda kwenye ngazi ya mashina na tawi ili kuhakikisha chama kinabaki na watu waaminifu na wema.

Maneno hayo ameyazungumza Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, Alhaji Abdallah Bulembo alipokuwa akizungumza na wanachama wa CCM wilaya ya Ilala katika ziara yake mkoni Dar es salaam.
“Kwanini tumepoteza madiwani ni usaliti tulioutengeneza ndani ya Chama chetu, kuwa CCM ni imani, kuwa muislam ni imani, na kuwa mkristo ni imani, sasa unapoona imani yako wewe ina utata kama unataka kwenda wewe nenda si ndio jamani, watakao kuwa na imani watazidi kubaki na imani yao,” alisema Bulembo.
Bulembo ameongeza kwa kusema anatambua kuwa Dar es salaam kuna shida na kuahidi kwamba kabla uchaguzi kumalizika uhakiki wa wasaliti wa chama utakuwa umekwishafanyika
“Kwahiyo kwa Dar es salaam tunayoshida na niliseme moja kwa moja hapa na popote ntakapo kwenda ntasema kabla ya agenda yangu kubwa ya uchaguzi Dar es salaam hatujamaliza na naomba nieleweke vizuri Dar es salaam hatujamaliza kuwahakiki waliokuwa wasaliti, tutakuja hadi kwenye matawi.” alisema Bulembo


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment