RAIS MAGUFULI ASIKIA KILIO CHA RIDHIWANI KUHUSU HALI YA UCHUMI NCHINI

Mbunge wa jimbo la Chalinze Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema kuwa amefurahishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa ni mwenye kusikia vilio vya watanzania wanyonge. Hayo ameyasema jana katika ukurasa wake wa Instagram kufuatia suali alilouliza Bungeni kwa wizara ya Fedha, Uchumi na Mipango juu ya hali ya uchumi ambayo inawabana watu wa chini.
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mhe. Ridhiwani Kikwete 

Mbunge huyo amejaribu kueleza namna mbali mbali ambazo zinaweza kuiezea mapato serikali bila ya kuwabana watu wa kipato cha chini, ikiwemo kupitia benki ya Uwekezaji TIB(Tanzania Investment Bank), TIBD (Tanzania Investment Development Bank) na miradi mbalimbali ukiwemo ule wa umeme wa bwawa la Kidunda,
Kufuatia hoja hiyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika ghafla ya ufunguzi wa mfumo mpya wa ukusanyaji kodi alisema kwamba anashangazwa kuona kuna wataalamu wengi wa uchumi lakini wanafikiria kuongeza kodi badala ya kufikiria namna nyingine ya kuongeza mapato ya nchi.
"Tuna wachumi wengi wamekaa tu. Wao wanawaza kupandisha kodi ya bia. Hawawazi nje ya mipaka namna mpya ya kuongeza mapato" amesema Rais Magufuli
Hoja hiyo ya Mbunge Ridhiwani imeonesha kuleta matumaini kwa kuwa ni miongoni mwa hoja ambazo Rais Magufuli amezisemea mapema zaidi mara baada ya kusikika bungeni.

Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment