AJIRA MPYA 10,184 ZIMETANGAZWA NA NYINGINE KUFUATA BAADAE

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Angellah Kairuki
Serikali kupitia Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imetangaza ajira 10,184 ikiwa ni vibali vya ajira kwa taasisi za umma, mashirika ya umma, serikali za mitaa, sekretarieti za mikoa, na wakala wa serikali ili kujaza nafasi zilizoachwa wazi kufuatia zoezi la uhakiki wav yeti feki ambalo liliwatoa watumishi takribani 15,000 kazini na kuacha nafasi hizo wazi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Angellah Kairuki ametangaza ajira hizo jana alipokuwa katika kikao na watumishi wa Umma wa Wilaya ya Kigamboni, amesisitiza pia kwa kusema kuwa utoaji wa vibali hivyo vya ajira umezingatia upungufu uliojitokeza baada ya kukamilika kwa zoezi la vyeti feki kwa watumishi wa umma kote nchini.


Waziri Kairuki ameongeza kuwa mpango wa Serikali wa kutoa ajira mpya bado upo pale pale na kuwa hawa watakaoajiriwa kujaza nafasi hizo watatakiwa kuripoti vituo vyao vya kazi mwezi Agosti mwaka huu.  Utaratibu wa kukamilisha idadi ya waajiriwa 15,000 wa nafasi zilizoachwa kutokana na zoezi la vyeti feki unaendelea ambapo mgao wa vibali vya ajira 4,816 ili kukamilisha nafasi 15,000. 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment