IGP SIMON SIRRO AFANYA MABADILIKO KWENYE JESHI LA POLISI, MPINGA AHAMISHIWA MBEYA


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Sion Sirro amefanya mabadiliko ya baadhi ya maofisa wa jeshi la polisi kwa kuwabadilishia sehemu za kazi maofisa hao. Maabadiliko hayo yamewahusisha kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani pamoja na Kamanda wa polisi Mkoa  wa Mbeya.

Ambapo aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Naibu kamishna wa Polisi Mohammed Mpinga amebadilishwa nafasi yake na kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya huku nafasi yake ikichukuliwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Fortunatus Musilimu.


Pia mabadiliko hayo yamemhusisha aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya (DCP) Dhahiri Kidavashari ambaye amehamishiwa makao makuu ya Jeshi la Polisi. 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment