EVERTON YATUA JIJINI DAR ES SALAAM KUKIPIGA NA GOR MAHIA YA KENYA

Kilabu ya Soka ya nchini Uingereza Everton imetua jijini Dar es salaam leo asubuhi kuikabili timu ya Gor Mahia kutoka nchini Kenya katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa utakaochezwa siku ya Alhamis Julai 13 katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Jopo la timu hiyo wakiwemo wachezaji hao na wakufunzi pamoja na maafisa wengine wa timu walifika uwanja wa ndege saa mbili asubuhi kutoka Liverpool. Mashabiki wengi wa soka ya England wamesafiri Tanzania kushuhudia Everton wakichuana na mabingwa wa Kenya, Gor Mahia katika uwanja wa taifa wa michezo jijini Dar es Salaam.
Wachezaji wa Timu ya Everton wakielekea kwenye basi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

Timu hiyo inaingia dimbani katika uwanja wa taifa ikiwa ni mara ya kwanza kwa timu hiyo kumchezesha mchezaji wake mpya straika Wyne Rooney ambaye amajiunga na timu yake hiyo ya zamani siku chache tu zilizopita akitokea Manhcester United ambako alikuwa akichezeka kwa kipindi cha miaka mitatu.
Timu hizo zote mbili, Gor Mahia ya Kenya na kilabu ya Everton zimewasili jijini Dar es salaam, huku timu ya Eeverton ikikaribishwa leo hii asubuhi na Waqziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe mara baada ya kutua katika uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere International Airport.
Aliyekuwa nahodha wa Manchester United na mchezaji wa Everton, Wyne Rooney akisalimiana na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dkt. Harisson Mwakyembe mara baada ya kuwasili katika uwanjua wa ndege wa JNIA jijini Dar es salaam leo asubuhi. 


Naye aliyekuwa nahodha wa Manchester United Wyne Rooney ameeleza kuwa amaefurahishwa na ujio wake nchini Tanzania kwa kuwa atapata fursa nzuri ya kuwatambua wachezaji wenzake wa timu hiyo ya Everton ambako maliko kwa sasa.
Mashabiki wa timu ya Everton wakipiga piacha na wachezaji wa timu hiyo akiwemo Rooney
 Wachezaji wa timu ya Everton wakiwa katika hoteli waliyofikia jijini Dar es salaam
Wachezaji wa timu ya Everton wakiwa katika shule ya Msingi Uhuru Jijini Dar es salaam
Wachezaji wa timu ya Everton wakisalimiana na wanafunzi wa shule ya Msingi Uhuru Jijini Dar es salaam

Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment