SPIKA JOB NDUGAI ATANGAZA RASMI NAFASI ZA KUGOMBEA UBUNGE

Spika WA Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai ametangaza nafasi nane za ubunge ambazo ziko wazi kuanzia sasa kufuatia kufutwa uanachama kwa wabunge hao na Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi CUF Prof. Ibrahim Lipumba, Mhe Spika amemuandikia Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ili aendelee na hatua zinazostahili kujaza nafasi hizo kwa Mujibu wa Sheria na Taratibu zilizopo.

Wabunge hao wamefukuzwa Uanachama kulingana na taratibu za Chama hicho na hivyo wamekosa sifa za kuendelea na Ubunge. Wabunge hao ni Mhe. Severina Silvanus Mwijage, (MB); Mhe. Saumu Heri Sakala, (MB); Mhe. Salma Mohamed Mwassa, (MB); Mhe. Riziki Shahari Mngwali, (MB); Mhe. Raisa Abdallah Mussa, (MB); Mhe. Miza Bakari Haji, (MB); Mhe. Hadija Salum Ally Al-Qassmy, (MB); na Mhe. Halima Ali Mohamed, (MB).
Mheshimiwa Spika amejiridhisha na maamuzi ya Mwenyekiti wa Chama hiko kwa mamlaka aliyonayo kwa kuzingatia kifungu cha 67(1)(b) cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 kikisomwa pamoja na kifungu 37(3) cha Sheria ya Uchaguzi Sura 343 kama ilivyojadidiwa Mwaka 2015.



Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment