WAZIRI MAKAMBA AVUNJA BARAZA LA MAZINGIRA (NEMC)

Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba ametengua uteuzi wa wajumbe wote saba wa bodi ya NEMC na kumteua Dkt. Elikana Kalumanga (UDSM) kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu.
Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba
Makamba amesema sababu za utenguzi wa baraza hilo ni Ucheleweshwaji wa kibali cha ukaguzi wa Mazingira, Tuhuma za rushwa katika usimamiz, Watendaji wa NEMC kusaidia baadhi ya watu wenye maslahi nao.
Waziri Makamba amesema kuwa waliitaka NEMC waeleze jinsi wanavyofanya kazi lakini hawakufanya hivyo.
Watendaji hao wamechukuliwa hatua baada ya uchunguzi wa kutosha huku hatua nyinginezo zikifuata baadae.
“kutokana na mapungufu makubwa ndani ya NEMC, tumeamua kuvunja bodi hii kuanzia leo na viongozi wengine tutawatangaza leo huku baadhi ya watendaji wa NEMC tumewasimamisha kazi ili ufanywe uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili kabla ya kuchukua hatua” amesema Makamba
Ameongeza kwa kusema kuwa kwa kuanzia sasa muwekezaji atakayekamilisha kutoa taarifa ya ujenzi wa kiwanda, ruhusa ya ujenzi itatoka ndani ya siku tatu tu, na kwamba wawekezaji wanaokwenda NEMC watatkiwa kuaznia kwa washauri elekezi ili kuondoa uhusiano wao na watu wa Baraza la NEMC.


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment