Jeshi la Polisi Tanzania limetoa
tahadhari juu ya kundi la watu walioibuka na kufanya utapeli kwa kujifanya
maafisa wa polisi kwa kigezo cha kuwapa ajira.
Imeelezwa kuwa watu hao
wamesambaza taarifa kupitia mitandao ya kijamii inayosomeka vigezo
sifa za kujiunga na jeshi la polisi huku ndani yake ikitaja sifa ambazo
kwa mujibu wa kikundi hicho ndizo anazopaswa kuwa nazo mtu anayeomba nafasi ya
kujiunga na jeshi la polisi.
Jeshi la polisi limewataka
wananchi wappuuzie taarifa hizo na kwamba jeshi la Polisi lina taratibu zake na
za wazi za kuajiri pale serikali inapotoa idhini ya kutangaza nafasi za ajira
na kuajiri.
0 comments:
Post a Comment