Paris
St-Germain(PSG) wamekamilisha usajili mshambuliaji wa Brazil, Neymar mwenye
umri wa miaka 25, kwa ada iliyoweka rekodi mpya ya ununuzi wa mchezaji ya Euro 222m
(£200m) kutoka Barcelona.
Rekodi
hiyo imeizidi mara mbili ya rekodi iliyowekwa na mchezaji Paul Pogba ambaye
alisajiliwa kwa £89m huku Neymar akiwa na dau kubwa zaidi la £200m.
Mchezaji
huyo kutoka timu ya Barcelona ya Hispania ametambulishwa rasmi katika timu ya Paris
St-Germain (PSG) na
kukabidhiwa jezi namba kumi na Mwenyekitin waklabu hiyo, utambulisho huo umefanyika
leo na umekuja mara baada ya Neymar kukubali dau nono la £200m.
Utambulisho
huo umefanyika leo mara baada ya mchezaji huyo kutua nchini Ufaransa ambako ndiko
makao makuu ya timu ya Paris St-Germain (PSG) akitokea nchini Hispania. Hivi karibuni
imeripotiwa kwamba baadhi ya maofisa wa
ligi ya Soka ya Hispania(La Liga) kuwa wamekataa maombi ya uhamisho wa mchezaji
huyo toka Barcelona kwenda Paris St-Germain (PSG).
Neymar
atakuwa analipwa euro 45m (£40.7m) kwa mwaka - euro 865,000 (£782,000) kila
wiki kabla ya kutozwa ushuru katika mkataba wake wa kwanza wa miaka mitano.
Hiyo ni jumla ya £400m.
![]() |
Rekodi ya viwango vya ada ya uhamisho tangu mwaka 1992
|
Neymar
amesema amejiunga na mojawapo ya klabu zenye ndoto kuu zaidi Ulaya na ameahidi
kufanya kila liwezekanalo kuwasaidia wachezaji wenzake.
"Ndoto
kuu ya Paris St-Germain ilinivutia kujiunga na klabu hiyo, pamoja na kujitoleza
kwao na nguvu zinazotokana na hili," amesema Neymar.
"Najihisi
niko tayari kuanza kazi. Kuanzia leo, nitafanya kila niwezalo kuwasaidia
wachezaji wenzangu wapya." Ameongeza Neymar
0 comments:
Post a Comment