![]() |
Chris Msando |
Chris Msando alikuwa msimamizi wa mifumo ya kompiuta kwenye
uchaguzi ambao utaandaliwa Jumanne, mifumo ambayo ingezuia wizi wa kura. Mwili wa Bwana Msando ulipatikana kwenye chumba kimoja cha kuhifadhia
maiti jijini Nairobi siku ya Jumatatu Julai 31.
Tukio hilo limetokea ikiwa imesalia wiki moja kabla ya
kuandaliwa uchaguzi mkuu nchini Kenya ambao utafanyika tarehe 8 Agosti.
Polisi wanasema kuwa mwili Msando pamoja na wa mwanamke ambaye
hakutambuliwa, ilipatikana eneo la Kikuyu lililo viungani mwa mji wa Nairobi na
kupelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha City Mortuary.
Mawasiliano ya mwisho kutoka mwa Musando aliyafanya siku ya
Jumamosi mwendo wa saa tisa alifajiri kupitia ujumbe wa SMS kwa mmoja wa
wafanyakazi wenzake.
0 comments:
Post a Comment