![]() |
Aliko Dangote |
"Ninaona
tarehe ya kukamilika ujenzi wa kiwanda hiki ni Disemba mwaka 2019, lakini
ninajua unaweza kuelewa kuwa ningependa mradi huu kukamilika mapema kuliko
ulivyopangwa," waziri alinukuliwa akimuambia Dangote alipotembelea mradi
huo mjini Lagos.
Kiwanda hicho kinatarajiwa kuwa ndicho kiwanda kikubwa zaidi cha
kusafisha mafuta duniani kinachojengwa eneo moja na cha pili kwa kutengeneza mbolea
duniani.
Licha ya kuwa mmoja wa wazalishaji wakubwa zaidi wa mafuta
duniani, Nigeria hununua asilimia kubwa ya mafuta kutoka nje na kwa sasa
inakabiliwa na uhaba mkubwa.
Wakati
ujenzi wa kiwanda hicho utakamilika kitakuwa na uwezo wa kusafisha mapipa
650,000 kwa siku kwenda petroli, gesi ,mafuta ya taa na ya ndege.
0 comments:
Post a Comment