MJUE RAIS AMBAYE HAJAWAHI KUUGUA KWA MUDA WA MIAKA 31

Kumekuwa na ripoti za kuugua kwa marais, hasa rais wa Nigeria Muhammadu Buhari, Robert Mugabe wa Zimbabwe na marais wengine barani Africa.
Kaguta Museven
Bwana Buhari amekuwa akipokea matibabu ya ugonjwa ambao haujulikani mjini London tangu mwezi Mei, ambayo ni ziara ya pili anafanya kupata matibabu nchini Uingereza mwaka huu. 
Lakini imekuwa tofauti kidogo kwa rais wa miaka mingi wa Uganda Yoweri Museveni, ambaye amenukuliwa akisema kuwa hajawai kuwa mgonjwa kwa muda wa miaka 31.
"Mshasikia kuwa Museveni ameugua au amelazwa hospitalini kwa miaka 31 iliyipota?" aliuliza Museveni.
"Hii ni kwa sababu ninafuata taratibu za kiafya ambazo zimenisaidia kuzuia baadhi ya magonjwa kama haya, mengi ya magonjwa hata yanazuiwa."
Baadhi ya marais ambao pia wamesafiri nchi za Ulaya, Asia na Marekani kupata matibabu tangu mwaka uliopita ni pamoja na marais wa Angola, Zimbabwe, Benin na Algeria.
Rais wa Zimbabwe ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 1980 amekosolewa na wapinzani kwa kuiongoza nchi "kutoka hospitalini" baada ya kufanya ziara ya tatu nchini humo kupata matibabu mwaka huu.


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment