UCHAGUZI WA WENYEVITI WA WILAYA CCM KURUDIWA TENA


Mkutano mkuu wa CCM taifa (NEC) umefuta uchaguzi wa wenyeviti katika wilaya nne baada ya kubaini wagombea waliojitokeza hawakuwa na sifa.

Akitangaza uamuzi huo leo katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Humphrey Polepole amezitaja wilaya hizo kuwa ni Moshi Mjini, Siha, Hai pamoja na Makete, "Nafasi za uenyekiti Wilaya za Hai, Siha, Makete na Moshi Mjini zitatangazwa tena wagombea wana kasoro kimaadili" amesema Polepole
Amesema sababu ya kufuta matokeo hayo ni kubainika kwamba wagombea waliojitokeza hwakuwa na sifa, pamoja na kubainika kuwepo kwa viashiria hatarishi kwa chama.
Aidha Polepole ameeleza hali ya uchaguzi wa chama hiko nchi nzima na kusema kuwa uchaguzi kwa ngazi ya mashina na matawi na kata umefanikiwa kwa asilimia 97, "Kwa nchi nzima CCM ina mashina zaidi ya laki 2 na 22 elfu na matawi zaidi ya 23 elfu Chaguzi zimekamilika zaidi ya 97%" amesema Polepole


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment