HAKUNA ALIYENUSURIKA KWENYE AJALI YA NDEGE DR CONGO

Ndege ya kijeshi imeanguka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuwaua abiria wote waliokuwamo kwenye ndege hiyo asubuhi ya leo.

Maafisa wa maswala ya anga wamesema kuwa ndege hiyo ilishindwa kupaa vizuri kutoka uwanja wa ndege wa N'djili katika mji mkuu wa Kinshasa na kuanguka katika makaazi ya Nsele.
Taarifa za awali kutoka mamlaka ya anga na maofisa wa jeshi wa DRC zimesema kuwa watu 12 wamefariki baada ya ndege hiyo ya mizigo ya Jeshi kuanguka muda mfupi baada ya kuruka
Taarifa PIA zimeeleza kwamba ndege hiyo ilikuwa imebeba magari mawili, silaha, raia kadhaa kutoka Urusi pamoja na maofisa wa kijeshi wa Congo
Mkurugenzi wa uwanja wa ndege wa Kinshasa George Tabora amesema kuwa ndege hiyo ilikuwa iimebeba mizigo na kwamba haikuwa na abiria wowote, "ndege hiyo haikuwa ikisafirisha abiria na hakuna aliyenusurika kwenye ajali hiyo" alisema Tabora


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment