POLEPOLE AWANYAMAZISHA KUHUSU KINANA

Katibu wa itikadi na uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole ametoa ufafanuzi kuhusu sababu zilizomfanya katibu mkuu wa chama hiko Mhe. Abdulrahman Kinana kutohudhuria kikao cha kamati kuu ya Chama hiko kilichofunguliwa na Mwenyekiti wake Dkt. John Pombe Magufuli hivi karibuni.
Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Humphrey Polepole
Polepole ametoa taarifa hiyo leo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za chama cha Mapinduzi, Lumumba jijini Dar es salaam na kusema kwamba katibu mkuu wa chama hiko Abdulrahman Kinana ameshindwa kuhudhuria kikao hiko kutokana na kuuguliwa na mwanafamilia wa karibu lakini alikuwepo wakati wa maandalizi ya mkutano huo.
"Katibu Mkuu Kinana anauguza mwanafamilia, ni mambo ya kifamilia lakini alikuwapo wakati wa maandalizi ya mkutano hadi mwisho," alisema Polepole
Aidha Polepole amekanusha taarifa zinazosambazwa na baadhi ya watu kuhusu Kinana, ya kwamba ameandika barua ya kujiuzulu, Polepole amesisitiza taarifa hizo kuwa ni za uzushi. 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment