SERIKALI IMESAINI MKATABA WA UJENZI WA RELI YA KISASA AWAMU YA PILI KUTOKA MORO HADI DODOMA

Serikali kupitia Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) imesaini mkataba wa ujenzi wa awamu ya pili wa Reli ya kisasa (STANDARD GAUGE RAILWAY) kutoka Morogoro hadi Makutupora yenye jumla ya urefu wa KM 422, ambapo ujenzi wake utagharimu jumla ya Dola za Kimarekani Bilioni 1.9 pamoja na kodi ya ongezeko la thamani na unatarajiwa kumalizika ndani ya miezi 36.

Tukio hilo limefanyika jana Sept 29 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwl. Nyerere (JNICC) jijini Dar es salaam ambapo waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa alishuhudia tukio hilo la utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa reli hiyo, ambapo Mkurugenzi wa Shirika la Reli na Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli Ndg. Masanja Kadogosa na Mkurugenzi wa Kampuni ya YAPI iliyoshinda kandarasi hiyo kutoka Uturuki waliweka saini makubaliano hayo.

Ujenzi wa awamu hii umetajwa kuhusisha ujenzi wa Kilomita 336 za njia kuu na Kilomita 86 za njia za kupishania treni na maeneo ya kupangiwa mabehewa ambao utafanya mradi huu kuwa na jumla ya Kilomita za reli 422, pia utahusisha ujenzi wa miundombinu ya umeme kutoka Morogoro hadi Makutupora, kwenye njia za kupishana na kupanga mabehewa ya treni, ujenzi wa vituo 8 ya abiria na vituo vine vya kupishania treni za mizigo.
Lakini pia mradi huu utahusisha ujenzi wa wigo wa wa njia ya reli kutoka Morogoro hadi Makutupora, ujenzi wa vivuko vya watembea kwa miguu, magari pamoja na sehemu maalum za kuvushia mifugo. Aidha reli hii itakuwa na uwezo wa kuhimili hadi tani 35 kwa ekseli, na kupitisha treni zenye uwezo wa kwenda mwendokasi wa Kilometa 160 kwa saa.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment