CATALONA KUFANYA MGOMO KUPINGA UKIUKWAJI WA HAKI ZAO



Mgomo mkubwa umeitishwa na vyama vya wafanyakazi huko Catalonia baada ya kuwepo kwa malalamiko mengi ya ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu ulioshuhudiwa wakati wa kura ya maoni ya siku ya Jumapili, mgomo huo unatishia kukwamisha shughuli sehemu kubwa za Catalonia kufuatia kura ya maoni yenye utata nchini Uhispania.

 Mamlaka nchini Uhispania zimeitaja kura hiyo ya maoni kuwa iko kinyume na sheria. Hata hivyo zaidi ya watu milioni 2.2 walipiga kura huku zaidi ya asilimia 90 ya waliopiga kura hiyo walitaka uhuru wa eneo hilo upatikane ili waweze kujitenga na nchi ya Uhispania.
Aidha mamia ya watu wameripotiwa kujeruhiwa wakati polisi wa Uhispania walipokuwa wakijaribu kuzuia zoezi hilo kuendelea, ambapo ilielezwa kuwa askari walitanda kila kukabiliana na watu waliofanya zoezi hilo siku ya Jumapili.
Baadhi ya maafisa walioamrishwa kuwazuia watu wasipige kura walionekana wakifyatua risasi za mipira, wakivamia vituo vya kupigia kura, kuwapiga watu kwa virungu na kuwavuta wanawake kwa nywele zao.
Polisi watatu walijeruhiwa siku ya Jumapili, kwa mujibu wa maafisa wa afya huko Catalonia. Mgomo huo wa leo Jumanne utavuruga shushuli za usafiri wa umma, shule na zahahati huko Catalonia.
Klabu maarufu ya soka ya Barcelona pia inatarajiwa kugoma, licha ya kuwa hawachezi mechi huku vyuo vya umma na makavazi nayo yakitarajiwa kugoma. Wachezaji wa timu hiyo walionekana siku ya Jumapili wamevalia mavazi ya kuashiria kutaka uhuru wa eneo hilo la Catalona. 
Ramani ikionesha mipaka na eneo la Catalona.

Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment