MAKUMBUSHO YA ODLUVAI GORGE YAZINDULIWA RASMI

Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan amezindua makumbusho ya Olduvai Gorge, ambako ni chimbuko la historia ya binadamu. Samia amesema kuwa makumbusho hayo ni kielelezo cha maisha na ustaarabu wa binadamu ambao unaelezea maisha ya vizazi vilivyopita, na kusaidia kujua hasa historia ya binadamu. Pia ameongeza kuwa ujenzi wa makumbusho hayo utasaidia kuvutia watalii na wanasayansi wa masuala ya mambo kale duniani.
“Makumbusho haya pia yatasaidia kujua sisi ni nani na tumetoka wapi,” amesema Makamu wa Rais.

Samia amesema eneo la Ngorongoro lina historia kubwa ya maisha ya zamadamu ikibainika miaka 3 milioni iliyopita walikuwepo walioishi kwa kutembelea miguu miwili na kuahidi kuwa serikali itaendelea kulihifadhi na kulilinda eneo hilo.
 “Hapa ni chimbuko la historia ya zamadamu, Serikali itaendelea kulihifadhi na kulitunza eneo hili,” amesema.
Makamu wa Rais ameishukuru Jumuiya ya Ulaya kwa kutoa fedha kugharimia ujenzi wa makumbusho hayo na miundombinu yake.
Makamu wa Rais ameitaka Wizara ya Maliasili na Utalii na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kuwa na mkakati wa kutangaza makumbusho hayo ndani na nje ya nchi ili kuvutia zaidi watalii.
Pia, amewaomba wananchi wa Ngorongoro kuendelea kuhifadhi eneo hilo ikiwemo kutopeleka mifugo eneo la Creta. Amesema Serikali inajitahidi kuwaondolea kero zao likiwemo tatizo la maji.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment