BRAZIL YAWA NCHI YA KWANZA KUFUZU KOMBE LA DUNIA 2018

Brazil imekuwa taifa la kwanza kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia ambazo zitachezewa nchini Urusi mwakani. Timu hiyo ilifuzu baada ya kulaza Paraguay 3-0, nao Argentina na Uruguay wakashindwa.
Brazil waliwashinda Paraguay kupitia mabao ya mshambuliaji wa Liverpool Philippe Coutinho, nyota wa Barcelona Neymar ambaye pia alipoteza mkwaju wa penalti na mchezaji wa Real Madrid Marcelo.
Brazil kwa sasa wamo alama tisa mbele ya Colombia ambao wanashikilia nafasi ya pili. Huo ulikuwa ushindi wa nane kwa Brazil chini ya Tite.
Paraguay, wamo alama chini ya nne bora, zikiwa zimesalia mechi nne kuchezwa.
Argentina wanakabiliwa na kibarua kufuzu baada ya kushindwa 2-0 na Bolivia na kushuka hadi nambari tano, alama moja nyuma ya Chile.
Uruguay, waliochapwa 2-1 na Peru mjini Lima Jumanne, wamo nambari tatu.
Taifa litakalomaliza nafasi ya tano litacheza mechi mbili za muondoano (nyumbani na ugenini) dhidi ya taifa kutoka Oceania.


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment