CARLOS, GAIDI KUTOKA VENEZUELA KUSHTAKIWA TENA



Carlos the Jackal, gaidi kutoka Venezuela, anayedaiwa kuhusika katika mashambulio kadhaa Ufaransa miaka ya 1970 na 80, atashitakiwa tena kuhusiana na shambulio lililotekelezwa katika duka moja. Mtuhumiwa huyo kwa sasa anatumikia vifungo viwili vya maisha jela kwa kufanya  mauaji kadha, kwa kile alichokidai kuwa ni kutetea haki za Wapalestina na wakomunisti ambapo katika mahojiano na gazeti moja, Ramirez anadaiwa kusema alitekeleza shambulio hilo kuishurutisha Ufaransa kumwachilia huru mwanaharakati wa kikomunisti kutoka Japan.
Ramirez mwenye umri wa miaka 67, atafikishwa mbele ya majaji watatu mahakamani mjini Paris Jumatatu kuhusiana na shambulio la guruneti lililotekelezwa katika jumba moja la kibiashara mtaa wa Latin Quarter mjini Paris Septemba 1974 ambapo watu wawili waliuawa na wengine 34 walijeruhiwa wakati wa shambulio hilo.
Ramirez amekanusha mashtaka hayo na wakili wake, Isabelle Coutant-Peyre, amesema kesi hiyo ni kupoteza wakati wa pesa bure.
Ramirez alipatikana na makosa mengine ya kutekeleza mashambulio manne ya mabomu mjini Paris na Marselle mnamo mwaka 1982 na 1983 ambapo watu kumi na moja waliuwawa na wengine mia moja na hamsini kujeruhiwa. ,Mnamo mwaka 2011 na 2013 alpatikana na hatia ya makosa hayo.
Ramirez alikamatwa mjini Khartoum na maafisa wa usalama wa Ufaransa mwaka 1994, miaka 20 baada yake kutekeleza shambulio lake la kwanza..
Wakili wa waathiriwa wa mashambulizi hay Georges Holleaux, amesema jamaa za waathiriwa wanasubiri sana na wangefurahia kumuona akiwa kizimbani. "Waathiriwa wamesubiri sana kumuona Ramirez akishtakiwa na kuhukumiwa. Vidonda vyao havijawahi kupona," amesema.


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment