WEZI WAVUNJA NA KUIBA NYUMBANI KWA JOHN TERRY

Inasemekana kuwa wezi wamevunja na kuingia katika nyumba ya aliyekuwa nahodha wa timu ya uingereza John Terry wakati akiwa katika likizo ya kifamilia.
John Terry ameripotiwa kuishi katika nyumba ya vyumba saba tofauti nchini humo.
Polisi Surrey wamethibitissha kutokea kwa tukio hilo siku za mwisho za juma lililopita kwenye nyuba ya mchezaji huyo iliyopo Oxshott. “Tunaweza kuthibitisha kuwa wizi ulifanyika katika nyumba moja iliopo Moles Hill ,Oxshott usiku wa terehe 25 na 26 mwezi Februari” alisema msemaji wa kituo cha polisi cha Surrey.
Wezi hao wanadaiwa kuvunja na kuuingia katika nyumba hiyo na kuiba vitu vyenye thamani wakati ambapo mchezaji huyo wa Chelsea mwenye umri wa miaka 36 akiwa likizo na familia yake akiwemo mkewe Toni kulingana na ripoti za gazeti la The Sun.


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment