DEWJI ASHINDA TUZO YA CEO BORA WA MWAKA 2017 BARANI AFRIKA

Mohammed Dewji
Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group), Mohammed Dewji ameshinda tuzo ya Afisa Mtendaji Mkuu Bora wa mwaka 2017 inayotolewa na Jukwaa la Wakurugenzi Watendaji Afrika (Africa CEO Forum). Dewji ameshinda tuzo hiyo kwa kuwashinda Abdulsamad Rabiu (CEO wa BUA Group), Issad Rebrab (CEO wa Cevital), Naguib Sawiris ( CEO wa OTMT Investments), Said Salim Awadh Bakhresa (CEO wa Bakhresa Group) na Strive Masiyiwa (CEO wa Econet). Akizungumza kuhusu ushindi huo, Dewji ameishukuru Africa CEO Forum kwa kutambua mchango wake kwa kumchagua kuwa mshindi tuzo hiyo lakini pia kuwashukuru Watanzania na Rais wa Tanzania, Dk. John Magufuli kwa kazi nzuri ya kudhibiti na kubana matumizi mabaya ya pesa ya umma. 

“Ninashukuru sana Africa CEO Forum kwa heshima hii ambayo mmenipa, napenda kutoa tuzo hii kwa nchi yangu Tanzania, bila wao nisingekuwa hapa na MeTL Group isingekuwa katika nafasi iliyonayo sasa, nawashukuru sana kwa kuniruhusu mimi na familia nzima ya MeTL kukua na kufika hapa, “Pia napenda kutoa heshima kwa Rais wangu John Pombe Magufuli anafanya kazi nzuri na wote tunajua Afrika inavyokabiliwa na vitendo vya rushwa lakini yeye ni mmoja wa watu ambao wanapambana na rushwa, kubana matumizi mabaya na wenye mwono katika kazi yake.” alisema Dewji. 

Aidha Dewji alisema kwa sasa bara la Afrika uchumi wake unakua kwa kasi huku akitolea mfano wa ripoti yam waka 2015 ambayo ilionyesha uchumi wa Afrika unakua kwa asilima 4 kwa mwaka kulinganisha na Ulaya inayokua kwa asilimia 1.5 hivyo kuwashauri wanachama wa Afrika CEO Forum kutumia vyema fursa hiyo kwa kufanya kazi kwa bidii na kuzisaidia nchi za Afrika kukua kiuchumi.


Tuzo za Africa CEO Forum zimetolewa Geneva, nchini Switzerland ambapo wanachama wa jukwaa hilo wapo katika mkutano wa siku mbili wakijadili mambo mbalimbali ambayo yanawahusu wao kama Watendaji Wakuu na jinsi gani wanaweza kulisaidia bara la Afrika.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment