Taarifa zinasema Bw Kaweesi na
walinzi wake wawili walioandamana nae wameuawa baada ya gari lake kumiminiwa
risasi na watu wasiojulikana alipokuwa akika nyumbani kwake Kulambiro, Kisaasi
kaskazini mashariki mwa mji mkuu Kampala.
Bw Kaweesi aliteuliwa kuwa msemaji wa polisi Agosti mwaka jana.
Taarifa zinasema alikuwa njiani
kwenda kuwahutubia wanafunzi katika chuo kikuu cha Uganda Christian University
alipokumbana na mauti yake. Wanafunzi walikuwa tayari wamekusanyika ukumbini
katika chuo hicho.
Aliyekuwa msemaji wa jeshi la polisi nchini Uganda |
Gari ambayo alikuwa amepanda Felix Kaweesi na walinzi wake wawiili
0 comments:
Post a Comment