Mwanamuziki
mkongwe wa Hip hop nchini Profesa Jay ametaja jina la albamu yake itakayokuja
pamoja na kumzungumzia Harmorapa ambaye kwa sasa amekuwa akiteka vichwa vya
habari.
Akiongea na kipindi
cha Twenzetu cha Times FM Jumatano hii, Jay amesema amepanga kuachia albamu
yake mpya ambayo itajulikana kama ‘The Icon’.
“Nimepanga
kuja na albamu. Mimi niliahidi kutoa albamu toka kitambo ila sasa niko busy tu
kutokana na majukumu ya hapa na pale ila nimejipanga kutoa albamu mpya na
itaitwa ‘The Icon’ kama ilivyo kwenye cover ya ngoma yangu mpya ‘Kibabe’ na
nyingine zitakazo kuja,” amesema rapper huyo.
Wakati
huo huo hitmaker huyo wa Kibabe, amemuongelea Harmorapa kwa kusema, “Watu
wasishangae kumuona Harmorapa akifika mbali maana kila msanii anapitia hustle
na yeye anahustle. Hivyo kufika mbali ni lengo la kila msanii na mimi napenda
kumheshimu kila msanii kutokana na jitihada zake.
0 comments:
Post a Comment