PICHA; RC MAKONDA AHOJIWA KUJIBU TUHUMA

Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda leo amefika mbele ya kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge kufuatia wito wa Kamati hiyo kumtaka afike mbele ya kamati kujibu tuhuma zinazomkabili za kuingilia Haki, Uhuru na Madaraka ya Bunge kutokana na matashi aliyoyatoa mapema mwezi februari 2017 jijini Dar es Salaam yaliyokuwa na madai ya kudharau Bunge. 

Wito wa kufika mbele ya Kamati hiyo unafuatia Azimio la Bunge lilitolewa tarehe 8 Februari 2017 ambapo Bunge liliazimia Mhe. Spika aweze kukubali Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexandra Mnyeti na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe Paul Makonda wahojiwe kutokana na Matamshi yao ya Kudharau Bunge


RC Makonda alipokuwa akiwasili bungeni na kupokelewa na Mkuu wa Kitengo cha Habari Bungeni, Owen Mwandumbya kuitikia wito wa Kamati ya Bunge


Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda akihojiwa  na Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga & Madaraka kujibu tuhuma zinazomkabili.

Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment